Udhibiti wa saratani

Mgonjwa akiandaliwa kwa matibabu ya Saratani

Udhibiti wa saratani unamaanisha kutibu ugonjwa wa saratani au kansa.

Saratani inaweza kutibiwa kwa kufanyia upasuaji, tibakemo, matibabu kwa njia ya eksirei, matibabu ya tibamaradhi, matibabu ya monokloni ya kingamwili au njia zingine. Uchaguzi ya matibabu hutegemea mahali uvimbe ulipo na daraja lake na hatua ya ugonjwa huo, pamoja na hali ya jumla ya mgonjwa (hali ya utendaji). Idadi kadhaa ya matibabu ya saratani ya majaribio hayajatengenezwa kikamilifu.

Kuondolewa kikamilifu kwa saratani bila kuharibu sehemu zingine za mwili ndilo lengo la matibabu. Wakati mwingine jambo hili linaweza kutimizwa kwa upasuaji, lakini hulka wa saratani ya kuvamia tishu zilizo karibu au kuenea kwenye maeneo ya mbali kupitia uenezi mdogo sana kiasi kwamba hauwezi kuonekana kwa macho mara nyingi huzuia ufaafu wake. Ufaafu wa tibakemo mara nyingi huzuiwa na kiwango cha kusumisha tishu zingine katika mwili. Mnururisho unaweza pia kuharibu tishu ya kawaida.

Kwa sababu neno "saratani // kansa" linarejelea jamii ya magonjwa,[1][2] hakuna uwezekano wa kuwa na aina moja ya "tiba ya saratani" zaidi ya kuwa na tiba moja ya magonjwa yote ya kuambukiza.[3]

Vizuizi vya Anjiojenesisi viliwahi kufikiriwa kuwa na uwezo wa kutkama matibabu ya "risasi fedha (silver bullet)" yanayoweza kutumiwa katika aina nyingi za saratani, lakini jambo hili halijadhihirika katika utendaji.[4]

  1. "What Is Cancer?". National Cancer Institute. Iliwekwa mnamo 2009-08-17.
  2. "Cancer Fact Sheet". Agency for Toxic Substances & Disease Registry. 2002-08-30. Iliwekwa mnamo 2009-08-17.
  3. Wanjek, Christopher (2006-09-16). "Exciting New Cancer Treatments Emerge Amid Persistent Myths". Iliwekwa mnamo 2009-08-17.
  4. Hayden, Erika C. (2009-04-08). "Cutting off cancer's supply lines". Nature. 458: 686–687. doi:10.1038/458686b.

© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search